Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Mha. MaryPrisca Mahundi (MB) akiskiliza wasilisho la taarifa ya utendaji wa Chuo cha Ustawi wa Jamii Kampasi ya Kisangara, kutoka kwa Meneja wa Kampasi hiyo Dkt. Leah Mwaisango ikiwa ni sehemu ya pili ya ziara yake ya kukagua na kupata taarifa ya Shughuli mbali mbali za Chuo cha Ustawi wa Jamii. Mhe. Mha. Naibu Waziri Mahundi katika ziara hiyo aliyoifanya tarehe 25 Februari 2026, aliambatana na Uongozi wa Wilaya ya Mwanga, Kamati ya Ulinzi na Usalama na Uongozi wa Kijiji cha Mbambua Kisangara, Mwanga.