Chuo cha Ustawi wa Jamii

MAADHIMISHO YA WIKI YA USTAWI WA JAMII

Watumishi wa Chuo cha Ustawi wa Jamii washiriki Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Ustawi wa Jamii yaliyofanyika katika viwanja vya Chuo cha Ustawi wa jamii, Kijitonyama, Dar es Salaam Agosti 30, 2025. Mgeni Rasmi alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania - Dkt. Philip Isdor Mpango akiwakilishwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum - Dkt. John Jingu. Aidha Mgeni rasmi alizindua Kampeni ya "PATA MSAADA WA KISAIKOLOJIA; IMARISHA AFYA YA AKILI" , Sera ya Taifa ya Wazee 2003 (Toleo la Mwaka 2024), Kitini cha Wawezeshaji wa Mafunzo ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto na Kitini cha Ufundishaji wa Watoa Huduma za Afya ya Akili, Msaada wa Kisaikolojia na Kijamii kwa Vijana Balehe.

WAZIRI WA MJJWMM MHE. DKT. DOROTHY GWAJIMA ATEMBELEA BANDA LA ISW KWENYE MAONESHO YA WIKI YA USTAWI WA JAMII

Mratibu wa kituo cha Elimu, Ushauri na Msaada wa Kisaikolojia, Rufina Khumbe akitoa maelezo kwa Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima alipotembelea banda la ISW katika Maonesho ya Wiki ya Ustawi wa Jamii 2025 yanayofanyika katika viwanja vya Chuo cha Ustawi wa Jamii.

KITUO CHA ELIMU, USHAURI NA MSAADA WA KISAIKOLOJIA KIMEWATEMBELEA WANAFUNZI WA KILUVYA SEKONDARI

Kuelekea Wiki ya Ustawi wa Jamii, Kituo cha Elimu, Ushauri na Msaada wa Kisaikolojia kilitembelea Shule ya Sekondari Kiluvya tarehe 9 Agosti 2025 na kuzungumza na wanafunzi wa Kidato cha Tano kuhusu mada za ukatili wa kijinsia, mahusiano na mawasiliano, pamoja na Career Guidance. Mada hizi ziliwasilishwa kwa mbinu shirikishi na zenye kuhamasisha ushiriki wa wanafunzi.

MKUU WA CHUO DKT. JOYCE NYONI ATEMBELEA BANDA LA ISW, MAONESHO YA NANENANE

Mkuu wa Chuo cha Ustawi wa Jamii, Dkt. Joyce Nyoni, ametembelea banda la #ChuoChaUstawiWaJamii katika Maonesho ya Nanenane yanayofanyika katika Viwanja vya Nzuguni, Dodoma, tarehe 8 Agosti 2025. Dkt. Nyoni alipokea maelezo kutoka kwa Mhadhiri Msaidizi Abubakar Fadhili na Mhadhiri Msaidizi Salama Limei kuhusu kozi ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto, pamoja na huduma za elimu na msaada wa kisaikolojia zinazotolewa kwa wananchi wanaotembelea banda hilo.

KOZI YA MALEZI, MAKUZI NA MAENDELEO YA AWALI YA MTOTO

Kwa mwaka huu wa masomo 25/26 Chuo cha Ustawi wa Jamii kinadahili kozi muhimu na yenye fursa nyingi za Kujiajiri na kuajiriwa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto kwa ngazi ya Certificate na Diploma ambayo inatolewa katika kampasi ya Kisangara, Mwanga pekee. Kozi hii itaandaa wataalam ambao watahakikisha mtoto anakuwa katika utimilifu wake; kiakili, kimwili, kijamii, kihisia, lugha, kiimani na kimaadili. Ili mtoto aweze kufikia utimilifu wake ni lazima apate afua mbalimbali ikiwa ni pamoja na afya, lishe bora, malezi yenye mwitikio, afua za ufunzaji wa awali, ulinzi na usalama, na uchangamshi wa awali. Wahitimu wa Kozi hii wanaweza kujiajiri lakini pia kuajiriwa katika maeneo mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kwenye vituo vya kulelea watoto mchana, vituo vya afya, katika dawati la mama na mtoto, makao ya watoto, kwenye madawati ya watoto, mashuleni, na kwenye mashirika yasio ya kiserikali ya kitaifa na kimataifa. Tunawakaribisha sana Wahitimu wa kidato cha nne na sita na wote ambao wangependa Kupata ujuzi adhimu wa kozi hii kufanya maombi ya Kozi hii pindi dirisha la awamu ya pili ya Udahili wa Certificate na Diploma utakapo funguliwa.

ZIARA YA KITAALUMA

Wanafunzi wa Chuo cha Ustawi wa Jamii watembelea kiwanda cha Kiboko Continuous Galvanizing Line kilichopo Mikocheni, Dar es Salaam. Lengo la ziara hii lilikuwa kuwawezesha wanafunzi kujifunza kwa vitendo kuhusu afya na usalama mahala pa kazi na kuona kwa karibu uhalisia wa yale wanayojifunza darasani.

Maonesho ya Sita ya Elimu ya Juu Zanzibar

Chuo cha Ustawi wa Jamii kilishiriki Maonesho ya Sita ya Elimu ya Juu Zanzibar, 14 Julai - 20 Julai 2025. Ilikuwa ni wakati mzuri wa Chuo kukutana na wanafunzi wa kidato cha sita wenye ndoto kubwa ya kujiendeleza kitaaluma.

Kikao Kujadili Afua kwa Watoto wa Mitaani

Wataalam wa Ustawi wa jamii kutoka Chuo cha Ustawi wa Jamii,Serikali ya Kata Ubungo, Wadau na Wazazi wakutana kujadili afua za watoto wanaoishi na kufanya kazi mtaani. Lengo la kikao hiki ni kuishirikisha jamii kuhusu kutatua matatizo yanayowakabili watoto hao na kuondokana na tatizo la watoto wanaoishi na kufanya kazi mitaani kupata ushirikiano wao, na kusikiliza maoni na mapendekezo kutoka kwao kuhusu namna bora ya kuwasaidia watoto wa mitaani kwa njia ya malezi, elimu, na msaada wa kijamii.

TEXAS UNIVERSITY WATEMBELEA ISW

Wahadhiri na wanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Texas, Marekani watembelea Chuo cha Ustawi wa Jamii kwa lengo la kuimarisha mahusiano ya kitaaluma na kutambua fursa za ushirikiano katika nyanja za utafiti, ubadilishanaji wa maarifa na maendeleo ya kitaaluma. Ziara hii ni hatua muhimu kuelekea kujenga ushirikiano wa kimataifa unaolenga kuinua ubora wa elimu inayotolewa taasisi.

HAFLA YA UTOAJI VYETI KWA WAHITIMU WA UANAGENZI

Naibu Mkuu wa Chuo cha Ustawi wa Jamii taaluma, Prof. Sotco Komba, amewatunuku vyeti wahitimu wa programu ya uanagenzi wanafunzi waliokamilisha mafunzo kwa vitendo katika taasisi mbalimbali. Prof. Komba amehimiza vijana kutumia fursa zilizopo chuoni na kutoa wito kwa taasisi mbalimbali kuendelea kutoa nafasi za mafunzo kwa vitendo ili kuwajengea uwezo wa kujiajiri. Nao Wamiliki wa taasisi wamekipongeza Chuo kwa kuanzisha programu yenye mchango mkubwa kwa maendeleo ya vijana, wakisisitiza umuhimu wa kuendelezwa. Aidha Wahitimu walitoa ushuhuda wa namna mafunzo hayo yalivyowawezesha kiujuzi na kitaaluma.

PROGRAMU ZA UBUNIFU, UANAGENZI NA USHAURI NASIHI NI FURSA ZA AJIRA KWA VIJANA: DKT. JINGU

Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. John Jingu amesema Programu za Ubunifu, Uanagenzi na Ushauri Nasihi ni fursa ya ajira kwa vijana nchini huku akiwahimiza vijana kutumia fursa hiyo ili wanapomaliza Chuo waweze kujiajiri na kuajiri wengine. Dkt. Jingu ameyasema hayo wakati wa ziara yake katika Chuo cha Ustawi wa Jamii Aprili 17, 2025 kukagua maendeleo ya mradi wa jenzi wa jengo la mihadhara na utoaji huduma Chuoni hapo. Katika ziara hii Dkt. Jingu amewasihi wanafunzi wa Chuo cha Ustawi wa Jamii kushiriki katika programu zinazotatua changamoto mbalimbali katika jamii ili elimu waliyoipata iweze kutoa matokeo chanya katika jamii. "Ninyi ni mainjinia wa kuleta mabadiliko katika jamii nimevutiwa sana na programu mnazoshiriki na kufanya hapa chuoni na kusema kweli ni nzuri sana" Ubunifu, Uanagenzi, Utoaji wa ushauri nasihi zote hizi ni fursa za ajira kwenu msizichukulie kimzaha" amesisitiza Dkt. Jingu. Aidha amewaasa wanafunzi kuongeza juhudi ya kusoma zaidi ya darasani ila pia kuendana na kasi ya utumiaji teknolojia kama vile akili bandia kutoa huduma na kuwa na mahusiano mazuri na wadau wa sekta washirika ambao ni muhimu kwao. Dkt. Jingu ameipongeza Menejimenti ya Chuo hicho kwa ubunifu katika kutoa elimu na Huduma za Kitaaluma hivyo kuendelea kwa Chuo kuonekana umuhimu wake kwa jamii na kuendelea kuwa kitovu cha ubora wa elimu na ujuzi unaoenda kutatua changamoto katika jamii na kuboresha maisha ya watanzania ambalo ndio lengo la Serikali ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. Pia Dkt. Jingu ametembelea mradi wa ujenzi wa ukumbi wa mihadhara na hatua za utekelezaji huku akisisitiza ubora na ukamilishwaji wa mradi kwa wakati. Kwa upande wake Mkuu wa Chuo cha Ustawi wa Jamii Dkt. Joyce Nyoni amesema Chuo kimeandaa mitaala mipya minne (4), itakayoongeza programu 15 za mafunzo katika fani mbalimbali ambapo Mitaala hiyo imepata ithibati na itaanza kutumika katika mwaka wa masomo 2025/2026.

Kamati ya Kudumu ya Bunge yakoshwa na Mradi wa Ukumbi wa Mihadhara ISW

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Fatma Toufiq, imetembelea mradi wa ujenzi wa ukumbi wa mihadhara #chuochaustawiwajamii kampasi ya Dar es Salaam tarehe 17 Machi, 2025. Baada ya ukaguzi kamati imeridhishwa na ubora wa mradi huo, muda na gharama iliyotumika ambapo ujenzi huo umefikia asilimia 38 ukijengwa kwa fedha za mapato ya ndani. "Mradi huu unatarajiwa kukamilika mwezi juni 2025, ambapo ukumbi huo utaweza kuhudumia wanafunzi 419 kwa wakati mmoja" alisema Dkt Joyce Nyoni - Mkuu wa Chuo ISW. Nimeridhishwa na maendeleo ya mradi huu na niwapongeze Mkuu wa Chuo Dkt Joyce Nyoni na menejimenti ya Chuo cha Ustawi wa Jamii kwa kazi nzuri ya Kusimamia mradi huo kwa Fedha za ndani alisema Mhe Fatma Toufiq - Mwenyekiti wa Kamati. Kamati imeahidi kuwasilisha bungeni pendekezo kwa serikali kuongezea fedha katika mradi huo ili fedha hizo zikasaidie katika ukamilishaji wa Ujenzi kwa haraka na katika ubora.

BODI YA MAGAVANA ISW YAKAGUA MAENDELEO KAMPASI YA KISANGARA

Bodi ya Magavana ya Chuo cha Ustawi wa Jamii Chini ya Uenyekiti wa Bi. Sofia Simba Leo tarehe 25 Februari, 2025 imetembelea na Kukagua Miradi ya maendeleo na Miundombinu ya Chuo cha Ustawi wa Jamii, Kampasi ya Kisangara, Mwanga, mkoani Kilimanjaro.Mwenyekiti wa bodi Bi. Sofia Simba pamoja na Wajumbe wa Bodi hiyo wameipongeza Menejimenti ya Chuo cha Ustawi wa Jamii kwa kazi kubwa iliyofanyika ya kukamilisha ujenzi wa Mabweni ya wanafunzi, bwalo la kulia chakula, kuongeza ofisi za watumishi na Kuongeza Wahadhiri pamoja na Watumishi waendeshaji katika kampasi ya Kisangara kama ilivyowasilishwa katika ripoti ya Meneja wa kampasi. Bodi ya Magavana imevutiwa zaidi na kukamilika kwa darasa mfano la kujifunzia la Kozi ya Malezi, Makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto inayotolewa katika kampasi ya Kisangara ambacho ni Kituo cha Umahiri wa Kozi hii. "Darasa mfano hili ni dogo kwa Ukubwa wa programu yetu na mahitaji ya ndani ya chuo pamoja na Kufundishia walezi na walimu wa shule za kulelea watoto zinazozunguka wilaya ya mwanga na Mkoa wa Kilimanjaro" alisema Dkt. Adolf Rutayuga Mjumbe wa Bodi ya Magavana. Mwisho Bodi imeshauri Menejimenti ya Chuo kuongeza Upandaji miti ili kuboresha mandhari na Mazingira ya Kampasi hiyo.

NACTVET WAFANYA UKAGUZI WA MIUNDOMBINU ISW

NACTVET watembelea Chuo cha Ustawi wa Jamii, Kampasi ya Dar es Salaam tarehe 19 Februari 2025 na kufanya tathmini na ukaguzi wa miundombinu ya chuo. Zoezi hili limefanyika ikiwa ni maandalizi ya NACTVET kutoa idhibati ya kuanzishwa kwa programu mpya za masomo katika Chuo cha Ustawi wa Jamii

BARAZA LA WAFANYAKAZI LAJADILI MUSTAKABALI WA ISW

Chuo cha Ustawi wa Jamii kimefanya kikao cha 19 cha Baraza la Wafanyakazi chini ya uenyekiti wa Mkuu wa Chuo, Dkt. Joyce Nyoni, 05 Februari, 2025 katika kampasi ya Dar es Salaam Kikao hiki kimewakutanisha wafanyakazi wa chuo pamoja na wawakilishi wa vyama vya wafanyakazi kwa ajili ya kujadili masuala muhimu ya maendeleo ya taasisi na ustawi wa wafanyakazi. Miongoni mwa ajenda zilizojadiliwa ni tathmini ya utekelezaji wa mipango na miradi 2024/2025 Washiriki wa kikao wamejadili kwa kina masuala haya kwa lengo la kuboresha mazingira ya kazi na kuhakikisha taasisi inaendelea kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

Kumbi za Mihadhara Kuongezwa ISW

Mkuu wa Chuo cha Ustawi wa Jamii, Dkt. Joyce Nyoni, amefanya ziara ya ukaguzi wa ujenzi wa madarasa mapya unaoendelea katika Kampasi ya Dar es Salaam, ambapo hadi sasa ujenzi huo umekamilika kwa asilimia 16 na unatarajiwa kukamilika rasmi ifikapo Mwanzoni mwa Mwaka 2025. Mradi huu unalenga kuboresha miundombinu ya kujifunzia katika kampasi ya Dar es Salaam.

Announcements
Joining Instructions 2025-08-21 15:22:20
CALL FOR PROPOSAL 2025-2026 2025-09-15 05:19:47
CALL FOR JOURNAL ARTICLES 2025-2026 2025-09-15 05:19:25
SELECTED CANDIDATES FOR ADMISSION INTO BACHELOR DEGREE PROGRAMMES-ACADEMIC YEAR 2025-2026 (ROUND ONE) 2025-09-03 06:13:10
SUPPLEMENTARY & SPECIAL EXAMS TIMETABLE FOR NTA 4 & 5. SEM II - 2024-2025. - Kisangara campus 2025-08-25 13:04:56
SUPPLEMENTARY & SPECIAL EXAMS TIMETABLE FOR NTA 4 & 5. SEM II - 2024-2025. - Kisangara campus 2025-08-25 07:09:20
SECOND SEMESTER, SPECIAL & SUPPLEMENTARY EXAMINATIONS TIME TABLE FOR NTA LEVEL 4 AND 5, SEPTEMBER INTAKE (2024/2025) ACADEMIC YEAR ) -MAIN CAMPUS 2025-08-20 13:26:33
TANGAZO KWA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA NA TAMISEMI 2025-08-18 14:42:21
CALL FOR APPLICATION FOR VARIOUS ACADEMIC PROGRAMMES-ACADEMIC YEAR 2025-2026 (SECOND ROUND) 2025-08-18 05:53:18
SELECTED CANDIDATES FOR ADMISSION INTO BASIC TECHNICIAN CERTIFICATE AND DIPLOMA PROGRAMMES ROUND 1 2025-08-14 14:47:37
JARIDA LA MTANDAONI APRILI - JUNI 2025-08-07 12:26:34
STUDENT'S ACCOMMODATION APPLICATION FORM 2025-07-02 12:31:54
ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA NA OFISI YA RAIS-TAMISEMI KUJIUNGA NA CHUO CHA USTAWI WA JAMII - 2025-2026 2025-06-17 07:34:57
TANGAZO - WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA NA TAMISEMI MWAKA WA MASOMO 2025-2026 2025-06-11 12:42:14
Jarida la Mtandaoni Januari - Machi 2025 2025-04-30 07:35:13
ALMANAC (2024-2025 ACADEMIC YEAR) 2025-03-28 10:35:35
Jarida la Mtandaoni Oktoba - Desemba 2025-01-22 05:10:45
Jarida la Mtandaoni July - September 2024 2024-10-31 12:48:49
FEE STRUCTURE-2024-2025 ACADEMIC YEAR 2024-08-26 10:11:55
Site Visitors
Today
563
Yesterday
1,418
This Week
9,692
This Month
44,752
All days
772,470
Online
2
Video