Chuo cha Ustawi wa Jamii

Maadhimisho ya wiki ya Ustawi wa Jamii 2023-12-03 16:51:19

Mhe.Dkt.Dorothy Gwajima atunuku tuzo mbali mbali katika mahafali ya 47 ISW

Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima (Mb) Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake na Makundi Maalum tarehe 8 Desemba, 2023 ametunuku tuzo mbali mbali kwa wahitimu katika Mahafali ya 47 ya Chuo cha Ustawi wa Jamii jijini Dar es Salaam. Katika mahafali haya wamehitimu wanafunzi 2,936 kati ya hao 1705 sawa na silimia 58 ni wanawake na 1327 sawa na asilimia 42 ni wanaume.

KONGAMANO LA 10 LA KITAALUMA LAJADILI ujenzi wa ujuzi na ushirikishwaji wa watu wenye wenye mahitaji maalum katika shughuli za maendeleo

Wadau, wanataaluma na wanafunzi wameshiriki katika kongamano la 10 la kitaaluma (Convocation) juu ya ujenzi wa ujuzi na ushirikishwaji wa watu wenye wenye mahitaji maalum katika shughuli za maendeleo. Akizungumza leo Desemba 7, 2023 jijini Dar es Salaam wakati akifungua kongamano hilo , Naibu Mkuu wa Chuo Prof.Sotco Komba Taaluma amesema chuo kimejikita zaidi katika maboresho ya watu wenye ulemavu ili kukuza ujuzi katika nyanja ya maendeleo ya kiuchumi ili waweze kushirikia michakato mbalimbali ya maendeleo katika taifa letu. Dkt. Nassib Mwaifunga, mtaalam wa masuala ya Uchumi na Fedha na Sheria kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu amewataka vijana kuchangamkia fursa mbalimbali kutoka ofisi ya Waziri Mkuu hasa walemavu ili waweze kujikomboa kiuchumi na kukuza maeneleo katika maisha yao ya kila siku. Aidha aliwataka vijana ambao ni wanafunzi kwenda na wakati katika mafunzo na masomo wanayochukua ili waweze kwenda na kasi ya soko la ajira duniani. Amebainisha fursa kubwa hasa ajira ambazo zinapewa kipaumbele kwa kuzingatia ujuzi iko katika kiwango kikubwa katika kozi za mafuta na gesi, usafirishaji, afya na vifaa tiba na madini. Mbali na hilo amewataka waajiri nchini kuachana na dhana ya kudharau watu wenye mahitaji maalum hasa katika kuwapa ajira kwani watu hao wana uwezo mkubwa wanapopewa nafasi. #chuochaustawiwajamii kimepongezwa kwa kuanzisha kitengo maalum utoaji wa huduma kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum na ni mfano wa kuigwa na vyuo vingine nchini Umekuwa ni utamaduni wa Chuo cha Ustawi wa Jamii kufanya kongamano hili la kitaaluma kila mwaka kabla ya mahafali yake, ambapo kwa mwaka 2023 mahafali hayo yatafanyika tarehe 08/12/2023 katika ukumbi wa JKT mwenge.

ISW Yashinda Tuzo Uandaaji Taarifa za Hesabu za mwaka 2022

Mkuu wa Chuo cha Ustawi wa Jamii Dkt. Joyce nyoni akiwa pamoja na baadhi ya wahasibu wa #ISW akipokea tuzo ya mshindi wa tatu ya uandaaji wa taarifa za hesabu chini ya viwango vya IPSASs 2022, katika kundi la vyuo vya elimu ya juu nchini kwa mara nyingine. Tuzo hiyo imetolewa jioni ya tarehe 1, Disemba 2023 na NBAA katika hafla maalum ya kutoa tuzo hizo.

BONANZA LA MICHEZO KUELEKEA KILELE CHA MIAKA 50 LAZINDULIWA

Dkt. Happy Mwakajila kwa Niaba ya Mkuu wa Chuo cha Ustawi wa Jamii Dkt. Joyce Nyoni amefungua Bonanza la Michezo ikiwa ni sehemu ya shughuli mbali mbali kuelekea Kilele cha Miaka 50 ya Chuo ambapo timu ya Mpira wa Miguu ya Wanaume #ISW imepimana nguvu na timu ya watumishi wa Hospitali ya Ocean Road Dar es Salaam ambapo timu zote mbili zimetoka sare ya bila kufungana katika mechi hiyo. Michezo hiyo itakutanisha Taasisi na vyuo mbali mbali ikihusisha wanafunzi na watumishi katika michezo mbali mbali.

NAIBU KATIBU MKUU WAKILI AMON MPANJU AFANYA KIKAO KIFUPI ISW

Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Wakili Amon Mpanju amefika katika Chuo cha Ustawi wa Jamii leo tarehe 10/11/2023 na kukutana na baadhi ya Wajumbe wa Menejimenti ya chuo ili kupata taarifa ya hali ya utoaji huduma, maendeleo ya miradi ya chuo na vile vile kutoa maelekezo na ushauri katika kuboresha utoaji huduma na utekelezaji wa miradi ya chuo.

CHUO CHA USTAWI WA JAMII CHAFANYA MAWASILISHO YA TAFITI ZA KITAALUMA.

Chuo cha Ustawi wa Jamii leo tarehe 10/11/2023 kimefanya mawasilisho ya tafiti mbili za kitaaluma ambazo imezifanya katika mada mbili tofauti ikilenga kutafuta kina cha suluhu ya matatizo ya hali mbali mbali yanayotokea katika jamii ya kitanzania. Akiwasilisha taarifa za tafiti hizo mmoja wa mtafiti kiongozi wa tafiti hizo Mhadhiri Mwandamizi Dkt. Zena Mabeyo amesema wamefanya tafiti mbili ambazo ni: - ‘’kuchunguza kanuni, maadili na mbinu zinazowalinda wanawake dhidi ya unyanyasaji Tanzania: uchunguzi kesi ya mikoa ya Mbeya, Mara na Tanga’’ na kuathirika kwa wafanyakazi wasio rasmi katika muktadha wa Uviko 19: kesi ya sekta ya utalii mkoani Kilimanjaro na Arusha. Kwa taarifa Zaidi tembelea ; https://www.isw.ac.tz/assets/doc/Dissemination_brief_PROWOMEN.pdf, https://www.isw.ac.tz/assets/doc/REPOA_FINAL_EDITED_POLICY_BRIEF_07_11_2023_(1).pdf

KARIBUNI - ISW

Mkuu wa Chuo cha Ustawi wa Jamii Dkt. Joyce Nyoni amefungua Mafunzo ya awali kwa watumishi wapya ISW. Akiongea katika ufunguzi wa mafunzo hayo katika kampasi ya Dar es Salaam, Dkt. Joyce amewapongeza watumishi hao wapya na kuwaasa kuwa waadilifu, wachapakazi, kufanya kazi kwa weledi, na kutoa huduma bora kwa wateja wa Chuo cha Ustawi wa Jamii.

Mkuu wa Chuo ISW Aongea na Wanafunzi wapya

Mkuu wa Chuo cha Ustawi wa Jamii Dkt. Joyce Nyoni amezungumza na Wanafunzi wapya wa Chuo cha Ustawi wa Jamii ambao wanatarajiwa kuanza mwaka wa masomo 2023/2024 katika wiki ya mafunzo ya awali na usajili ambayo inaendelea Chuoni hapa. Amewapongeza kwa kuweza kuchaguliwa na kupata nafasi ya kujiunga na elimu ya Juu na hasa Chuo Cha Ustawi wa Jamii. Dkt. Joyce alisema tunatamani kuwa na ninyi mpaka mwisho wa Programu zenu za masomo yaan kutoka Cheti, Diploma mpaka Degree. "Tufike mwisho wa safari kwa ushindi bila majeraha, majeraha ni kurudia somo au kufeli somo na kulibeba mwaka unaofuata. Mimi nilimaliza Masomo yangu bila Kufeli Somo na ninyi mnaweza" alisema Dkt. Joyce Tuweke malengo ya kumaliza bila majeraha,tumalize shule kwa wakati ili tusiwape mzigo wazazi na walezi wetu ambao wana tuwezesha kulipa ada na mahitaji tukiwa masomoni. Kama Chuo tuna ahidi kuwapa huduma stahiki, za kitaaluma na Kiutawala, nawasihi sana tumieni vizuri ofisi zetu kupata ushauri pale mnapopata changamoto zozote, tuna Kituo cha Elimu,Ushauri na Msaada wa Kisaikolojia, Ofisi ya Mshauri wa wanafunzi, Dawati la Jinsia, pamoja na Ofisi za Wakuu wa Idara zenu, muwe huru kwenda kupata huduma. Mwisho nawaomba muwe mabalozi wazuri wa Chuo chetu, Mvae vizuri, Muwe nadhifu, na Muongee vizuri na Jamii yenu kama wasomi wa Chuo cha Ustawi wa Jamii

Registration & Orientation Week at ISW

As the first week of Registration and Orientation takes Course ISW Congratulates and Welcomes our new students to both our Campuses and we assure you a great experience of our Administrative and Academic services. Newly Selected Students are supposed to report at the Institute (both Campuses-Dar es Salaam and Kisangara) for registration and orientation as follows: - 16th October, 2023 -NTA Level 4 (Basic Technician Certificate) and NTA level 5 (Technician Certificate) students and on 23rd October, 2023 -NTA LEVEL 7 (Bachelor Degree) students.

KOICA, ISW WAKABIDHIANA NA KUZINDUA VIMBWETA

Mkurugenzi Mkaazi wa KOICA Tanzania Mr. Manshik Shin na Mkuu wa Chuo cha Ustawi wa Jamii Dkt. Joyce Nyoni tarehe 04, Oktoba 2023, wamekabidhiana na kuzindua matumizi ya vimbweta vipya vilivyojengwa katika eneo cha Chuo cha Ustawi wa Jamii Kampasi ya Dar es Salaam. Hafla ya makabidhiano hayo imefanyika baada ya ujenzi wa vimbweta hivyo kukamilika ambapo KOICA kupitia mradi wao wa kujitolea ulifanikisha kujengwa kwa vimbweta hivyo vya kisasa ambavyo vitapunguza uhaba wa sehemu za kujisomea wanafunzi wakisubiri vipindi au wakati wa mitihani. KOICA kwa muda sasa imekuwa mshirika wa karibu wa maendeleo wa Chuo cha Ustawi wa Jamii ambapo mpaka sasa wameshafanya miradi kadhaa katika kuboresha miundombinu na mazingira ya utoaji huduma katika chuo cha ustawi wa jamii.