Chuo cha Ustawi wa Jamii

CHUO CHA USTAWI WA JAMII CHAONGEZA MDAU MASHIRIKIANO YA KITAALUMA KIMATAIFA

Chuo cha Ustawi wa Jamii tarehe 27 Septemba, 2023 kimesaini makubaliano ya mashirikiano ya kitaaluma na chuo cha theolojia na sayansi za jamii cha Friedensau University kutoka nchini Ujerumani. Makubaliano hayo yamesainiwa na Dkt. Joyce Nyoni Mkuu wa Chuo cha Ustawi wa Jamii na Prof Ulrike Schultz Mkuu wa Kitivo cha Sosholojia ya Maendeleo na Uchumi kutoka Chuo cha Theolojia na Sayansi za Jamii Friedensau cha nchini Ujerumani. Katika makubaliano hayo vyuo hivi viwili vimekubaliana kushirikiana ili kuwezesha kubadilishana wanafunzi ikiwa ni pamoja na kuwezesha mafunzo ya kimataifa na, au wanafunzi kusoma muhula nje ya nchi. Makubaliano mengine ni; ufundishaji na ukuzaji wa mitaala, kubadilishana uzoefu wa vitivo vya kitaaluma ikijumuisha kutembeleana na ukuzaji wa uwezo kitaaluma, utafiti wa pamoja na uchapishaji wa kitaaluma.

Menejimenti, Watumishi ISW Wanolewa Mfumo mpya Manunuzi ya Umma ( NeST)

Mkuu wa Chuo cha Ustawi wa Jamii Dkt. Joyce Nyoni amefungua mafunzo ya mfumo mpya wa manunuzi ya Umma yaani (NeST) kwa Menejimenti na watumishi wa Chuo Cha Ustawi wa Jamii ambayo yamewezeshwa na wataalam kutoka PPRA (Public Procurement Regulatory Authority). Mafunzo hayo ya Siku 5 yalifanyika kuanzia tarehe 18-22/09/2023. Katika mafunzo hayo, watumishi pamoja na menejimenti ya Chuo cha Ustawi wa Jamii wameweza kufahamu umuhimu wa teknolojia kwenye ununuzi wa Umma, mafanikio na changamoto ya teknolojia kwenye mfumo wa zamani Taneps na maboresho makubwa yaliyofanywa katika mfumo mpya wa (NeST).

ISW Yaendesha Mafunzo ya Uwekaji Digiti katika Maktaba na Mifumo ya Taarifa

Chuo cha Ustawi wa Jamii tarehe 18-22 Septemba, 2023 kimeendesha mafunzo ya digitali kwa maktaba na taasisi za taarifa. Mafunzo hayo yalihudhuriwa na wakutubi, watafiti kutoka taasisi mbali mbali za serikali. Mada hii Pia iligusia nyanja muhimu za kidigitali kama muundo wa mafaili ya kidigitali na zana zake, mbinu zinazotumika, mchakato wa kupanga digitization, viwango vya metadata, masuala ya digitization na hakimiliki, tathmini ya digitization, muhtasari wa FOSS kwa ajili ya mradi wa digitization, muhtasari wa DSPACE na hazina ya utafiti. Mafunzo haya yaliandaliwa na kuwezeshwa na wataalam wa idara ya huduma za maktaba ISW.